Huku taifa la Kenya likikaribia uchaguzi mkuu utakaofanyika agosti 8, Taarifa zimeibuka kupianga kustaafu kwa Rais Uhuru Kenyatta.
Rais Kenyatta amehudumu kama Rais Wa nne wa Jamhuri ya Kenya kwa vipindi viwili mtawalia.
Akitarajiwa kustaafu uongozini hivi karibuni, Rais Kenyatta ahapa kuacha taifa la Kenya kwa Amani huku akitoa pendekezo lake kwa Kiongozi Bora atakayemrithi na atakayeendeleza urithi wake.
Akibaini, katibu Mkuu Wa chama Cha wafanyikazi nchini Kenya Francis Atwoli ametoa madai kwamba Rais Kenyatta Hatastaafu kama Rais Wengine hapo awali.
Bwana Atwoli amesisitiza kwamba, Rais Kenyatta atasalia serikalini kama msemaji mkuu.
Akitetea madai yake, Bwana Atwoli amesema kuwa, ililichukua taifa Kenya takribani miaka ishirini kupata msemaji mkuu wakati mwanzilishi wa taifa la Kenya na Rais Wa kwanza hayati Mzee Jomo Kenyatta alipofariki.
Madai ya bwana Atwoli yaonekana kinyume na sheria kwa kuzingatia maelezo ya katiba ya mwaka wa 2010.
Aidha, wapinzani wa Rais Kenyatta wamepinga hatua hiyo huku wakimtaka Rais Kenyatta kustaafu punde kipindi chake uongozini kitakapomalizika.
Hata hivyo, Naibu Rais William Ruto na wandani wake wakiwemo Kiongozi wa chama Cha ANC Musalia Mudavadi and wa Ford Kenya Moses Wetangula wamemsuta Rais Kenyatta kutokana na mpango wake wa kumuidhinisha aliyekuwa Waziri Mkuu Wa Zamani Raila Odinga kama mrithi wake.
Tembelea tovuti www.stateupdate.co.ke kupokea habari zaidi